Tuesday, 27 December 2016

JESHI LA POLISI LAZUIA ZAIDI YA MABASI 50 KUSABIRISHA ABIRIA

Jeshi la Polisi, Kikosi cha Usalama Barabarani limezuia zaidi ya mabasi 50 kusafirisha abiria kwenda Mikoani kutokana na makosa mbalimbali huku mengine yaking'olewa namba kabisa kutokana na kuwa na hitilafu nyingi na hivyo kutakiwa kurudishwa gereji kwanza kwa ajili ya kufanyiwa matengenezo makubwa.

KAMANDA MPINGA AKIELEZEA MADEREVA WALIOONGOZA KWA KUTUMIA KILEVI DSM KIPINDI CHA XMAS

Kamanda wa polisi Kikosi cha Usalama barabarani, DCP Mohammed Mpinga ametoa takwimu za madereva walevi mkoa wa DSM msimu huu wa Sikukuu za  Christmass

Tuesday, 13 December 2016

PICHA NA MATUKIO YALIYOJIRI KATIKA MASHINDANO YA FAINALI: MPINGA CUP


PICHA NA MATUKIO

Mmoja wa Waratibu wa Mashindano ya Mpinga Cup 2016, Insp Aghata Mashayo wa pili kulia, akifuatilia kwa makini Fainali ya Mashindano ya mwaka huu.
 
 Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani mohammed Mpinga, (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha na viongozi mbali mbali  wakati wa Fainali ya Mpinga Cup 2016. iliyofanyika kwenye uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani mohammed Mpinga, (kulia) akifafanua jambo wakati wa Fainali ya Mpinga Cup 2016. iliyofanyika kwenye uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.
 

MATUKIO NA HABARI YALE YALIYOJIRI KATIKA FAINALI ZA MPINGA CUP

Mratibu wa Mpinga Cup 2016 ASP Mbuja Matibu  akimkaribisha Uwanjani Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani mohammed Mpinga, wakati wa Fainali ya Mpinga Cup 2016.