Monday, 10 October 2016

PICHA NA MATUKIO YALIYOJIRI KATIKA SIKU YA UZINDUZI WA WIKI YA NENDA KWA USALAMA BARABARANI KITAIFA MKOANI GEITA



Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto)
akimpa zawadi ya Kombe la Ushindi wa kwanza Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam, Veronica Innocent, ambaye alishinda nafasi ya kwanza katika uchorani wa picha zinazoonyesha usalama barabarani ambayo zilipambanishwa katika shule za Mkoa wa Dar es Salaam na Geita. Masauni aliyazindua Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani, ambayo yanafanyika Kitaifa, katika Viwanja vya CCM Kalangalala, mjini Geita. Masauni katika hotuba yake aliwaagiza Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) kuyaondoa matuta yote yaliyopo katika Barabara Kuu na aliwataka madereva wote nchini kufuata sheria za usalama barabarani ili kupunguza ajali za kizembe. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment